Accessibility Settings

Text Size

Color Contrast

Language

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Kilimo

Kampuni ya Mbolea Tanzania

/ News

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Mbolea Tanzania, Bw. Samuel Mshote, akisimamia ufungashaji wa Mbolea tayari kupelekwa kwa wakulima.

Imewekwa: 28 January, 2026
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Mbolea Tanzania, Bw. Samuel Mshote, akisimamia ufungashaji wa Mbolea tayari kupelekwa kwa wakulima.

Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) imeendelea kutekeleza mkakati wa Serikali wa kuhakikisha upatikanaji wa mbolea kwa wakati kwa wakulima nchini, kufuatia uingizaji wa tani 50,000 za mbolea aina ya DAP kwa ajili ya msimu wa kilimo unaoendelea. Hatua hii inalenga kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao na kuimarisha usalama wa chakula nchini.