TFC yelekezwa kuimarisha upatikanaji wa Mbolea kwa Wakulima
Imewekwa: 04 May, 2026
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayesimamia Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula, Prof. Peter L. Msoffe, ameielekeza TFC kuimarisha upatikanaji wa mbolea ili kuhakikisha uzalishaji wa kilimo haukatizwi, akisisitiza kuwa usalama wa chakula ni kipaumbele cha taifa.
Pia ameitaka TFC kushirikiana na Halmashauri kuzalisha mbolea za asili kutokana na taka na kuvutia wawekezaji kuongeza uzalishaji wa ndani. Mkurugenzi Mkuu wa TFC, Bw. Samuel Mshote, ameahidi upatikanaji wa mbolea kwa wakati licha ya changamoto za nje.

