Ziara ya Bodi ya TFC Kuhamasisha Matumizi Sahihi ya Mbolea na Shamba Darasa
Imewekwa: 13 December, 2025
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi, Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC), wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi, Dkt. Florens Turuka (wa pili kutoka kushoto), Novemba 25, 2025 wametembelea kituo cha mauzo cha Tunduru, Mkoa wa Ruvuma ili kuona hali ya mauzo ya mbolea mkoani hapo.
Katika ziara hiyo, Dkt. Turuka amesisitiza juu ya utoaji wa elimu ya matumizi sahihi ya mbolea na kuelekeza kuwa na shamba darasa la mfano, ili wakulima wajifunze kwa vitendo jinsi mbolea za TFC zinavyozalisha mazao kwa tija.

