Accessibility Settings

Text Size

Color Contrast

Language

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Kilimo

Kampuni ya Mbolea Tanzania

/

OMBI LA KUONESHA NIA (EOI) YA KUWEKEZA KUPITIA UTARATIBU WA UBEBAJI WA PAMOJA WA BIASHARA (JOINT VENTURE)

Imewekwa: 31 August, 2026

OMBI LA KUONESHA NIA (EOI) YA KUWEKEZA KUPITIA UTARATIBU WA UBEBAJI WA PAMOJA WA BIASHARA (JOINT VENTURE)

1. Kampuni ya Tanzania Fertilizer Company Limited (TFC) ilianzishwa tarehe 6 Julai 1968 chini ya Sheria ya Makampuni (Companies Ordinance - CAP 212), ambayo sasa inajulikana kama Sheria ya Makampuni (Companies Act, R.E. 2023), kupitia Cheti cha Usajili Namba 4335. TFC ni taasisi ya serikali iliyo chini ya Wizara ya Kilimo, yenye jukumu la kusaidia maendeleo ya kilimo nchini kupitia shughuli za uzalishaji, uingizaji nchini, uchanganyaji, usambazaji, na uuzaji wa mbolea pamoja na pembejeo nyingine za kilimo kwa wakulima kote nchini.
2. TFC inakusudia kuendeleza eneo lake (Kiwanja Na. 448), lililopo kando ya Barabara ya Chole, Oyster Bay, Masaki, Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam, lenye ukubwa wa mita za mraba 4,432. Eneo hilo la mradi lipo katika viashiria vya eneo (coordinates) (-6.7441041, 39.2809438), takriban kilomita 14 kutoka katikati ya jiji (CBD), katika eneo la kimkakati linalojulikana kwa miradi ya thamani kubwa ya kibiashara na makazi.
3. TFC inatafuta wawekezaji wenye sifa nzuri na uaminifu ili kushirikiana nao kupitia utaratibu wa Ubia wa Biashara (Joint Venture - JV) kwa ajili ya kubuni, kufadhili, kujenga, kuendesha/kutunza, na hatimaye kukabidhi jengo la ghorofa 15 (G+14) lenye matumizi mchanganyiko ya kibiashara na makazi. Jengo hilo litajumuisha eneo la maegesho ya magari chini ya ardhi (basement), maeneo ya maduka na biashara katika ghorofa ya chini, ofisi katika ghorofa ya 1 hadi ya 4, mchanganyiko wa ofisi na makazi katika ghorofa ya 5 hadi ya 12, na nyumba za makazi za hadhi ya juu katika ghorofa za juu. Dhana hii ya uendelezaji inatoa mwongozo unaonyumbulika unaowaruhusu wawekezaji kupendekeza miundo bunifu ya usanifu na mipangilio yenye tija kibiashara, ikizingatia dira ya TFC ya kuwa na jengo la kisasa lenye matumizi mchanganyiko katika eneo la kimkakati.
4. Tangazo hili linatoa wito wa kuwasilisha maombi yaliyofungwa (sealed submissions) ya Kuonesha Nia (EOI) kutoka kwa wawekezaji wenye sifa na uaminifu, wanaotaka kuonesha nia yao rasmi ya kuwekeza katika kiwanja hicho kupitia Ubia wa Biashara kwa utaratibu wa Kubuni, Kujenga, Kufadhili, Kuendesha/Kutunza na Kukabidhi (DBFOMT). Wawekezaji wenye nia na sifa stahiki lazima wawasilishe maombi yao ya Kuonesha Nia yakiambatana na taarifa za kina zifuatazo:
(a) Barua ya kuonesha nia;
(b) Wasifu wa kampuni na nyaraka zilizothibitishwa za usajili, zikiwemo lakini zisizoishia kwenye... Hati ya Makubaliano na Kanuni za Chama/Kampuni (MEMARTS), Cheti cha Usajili wa Kampuni, Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN), na usajili wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT);
(c) Ripoti ya Utafiti wa Uwezekano wa Mradi;
(d) Muundo wa awali wa dhana ya mradi unaopendekezwa wa matumizi mchanganyiko;
(e) Makadirio ya kina ya gharama;
(f) Makadirio ya mapato;
(g) Uthibitisho wa uwezo wa kifedha, ikijumuisha taarifa za benki za miezi sita, na aidha Barua ya Kuthibitisha Uwezo wa Kifedha au Barua ya Ahadi kutoka benki au taasisi ya fedha inayoaminika;
(h) Taarifa za fedha zilizokaguliwa kwa miaka mitatu (3) iliyopita; na
(i) Uthibitisho wa utaalamu, ujuzi, na uzoefu unaohusika, ikiwemo kukamilisha kwa mafanikio angalau miradi mitatu (3) ya uendelezaji wa majengo inayofanana na huo ndani ya miaka kumi (10) iliyopita.
5. Wawekezaji wa ndani au wa kimataifa wenye nia na sifa zinazostahiki wanaweza kuwasilisha 'Taarifa ya Nia' (Expression of Interest) kama kampuni moja au kama muungano wa kampuni mbili au zaidi.

6. Mpango wa ufadhili uliowasilishwa lazima uambatane na uthibitisho wa upatikanaji wa fedha kwa ajili ya mradi unaopendekezwa, kwa njia ya taarifa za benki, ahadi ya mkopo (line of credit) kutoka taasisi ya fedha inayoaminika, au ushahidi mwingine wowote unaokubalika.
7. Ombi lolote la ufafanuzi LAZIMA lifike ofisi ya Mkurugenzi Mkuu kabla au kufikia siku saba (7) kabla ya tarehe ya mwisho ya kuwasilisha 'Taarifa ya Nia'.
8. TFC inahifadhi haki ya kukubali au kukataa wasilisho lolote, na kufuta mchakato wa 'Taarifa ya Nia' pamoja na kukataa mawasilisho yote wakati wowote kabla ya hatua ya kuchagua orodha fupi na kutoa zabuni, bila kuwajibika kwa namna yoyote kwa waombaji walioathirika.
9. Tangazo hili la 'Taarifa ya Nia' limetolewa tarehe 14 Agosti 2026 na litakuwa wazi kwa ajili ya kuwasilisha maombi
hadi tarehe 14 Septemba 2026 saa 9:30 alasiri. Maombi yanapaswa kuelekezwa na kuwasilishwa kwa:

Mkurugenzi Mkuu,
Tanzania Fertilizer Company (TFC),
TFC House, Mtaa wa Ubungo NHC, Nyumba Na. UB/NHC/729,
S.L.P. 9434, 
DAR ES SALAAM,TANZANIA

 

 

slot gacor